Vidonda vya Tumbo


 *VIDONDA VYA TUMBO*, au *GASTRIC ULCERS*, ni majeraha yanayotokea kwenye ukuta wa ndani wa tumbo.


🌳Husababishwa na kushuka kwa kiwango cha ute (mucus) unaolinda kuta za tumbo dhidi ya asidi kali inayozalishwa kwa ajili ya kumeng'enya chakula.


🌳Hali hii hufanya sehemu za kuta za tumbo kuwa wazi na kuathirika, na hivyo kusababisha majeraha au vidonda.


*Hizi ni dalili za vidonda vya tumbo (Gastric Ulcers):-*

👉 Maumivu makali ya tumbo, hasa sehemu ya juu.

👉 Kiungulia (hali ya kuchomachoma kifuani).

👉 Kichefuchefu na kutapika.

👉 Kutapika damu au kutapika vitu vyenye rangi ya kahawia.

👉 Kinyesi chenye rangi nyeusi au kinachoonekana kama lami.

👉 Kupoteza uzito bila sababu maalum.

👉 Kukosa hamu ya kula.


NB: Vidonda vya Tumbo vikikaa kwa muda mrefu bila matibabu kamili, vinaweza kupelekea Kansa/ Cancer ya Tumbo


Post a Comment

0 Comments